Saturday 6 April 2013

ANGALIA PICHA ZA DEREVA BODABODA ALINUSURIKA KUFAA BAADA YA KUGONGWA NA TRENI, MOROGORO

Kijana aliyegongwa na treni akiwa kwenye gari pamoja na wasamalia tayari kuwaishwa hospitali baada ya ajali.
Pikipiki iliyogongwa baada ya ajali, pembeni ni kofia ngumu aliyokuwa amevaa dereva ikiwa imevunjika.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo akiangalia kofia ngumu aliyokuwa amevaa dereva wa bodaboda.
Pikipiki ikiondolewa eneo la ajali.
 KIJANA mmoja ambaye jina lake halikufahamika mara moja, juzi (Jumatano) aalinusurika kifo baada ya kugongwa na treni akiendesha bodaboda eneo la Nunge mkoani Morogoro. Kijana huyo aliyekuwa na pikipiki yenye namba za usajili T 859 BDU inadaiwa kuwa alikuwa akiwaisha chakula kwa ajili ya mgonjwa aliyelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro.

No comments:

Post a Comment